Nasikia
kuchemka ndani yangu... uuh! Sikia usimtendee mtu mema eti kwasababu
alishawahi kukutendea mema, usionyeshe upendo kwa mtu kwasababu tu na
yeye anaonyesha upendo kwako, usisaidie mtu kwasababu alishawahi
kukusaidia au unategemea siku moja na wewe ukiwa na shida atakuja
kukusadia... kwa kufanya hivyo hakuna tofauti yoyote, maana hata wana wa
dunia hii hufanya hivyo hivyo... Sisi tumeshabadilishwa
nia zetu na kuwa kama Kristo, hatufanyi tena kwa namna ya dunia hii..
maana hata Baba yetu wa mbinguni huwanyeshea mvua waovu na wema(Matt
5:45).. huwa habagui aah! Tunatakiwa kutenda mema wakati wote bila
kuangalia upande wa pili walishatutendea mema au la, tuwe na upendo..
tuwapende adui zetu na kuwaombea wanaotuudhi(Matt 5:44).. tusaidie hata
wale ambao hawatusaidii, na tunaposaidia tusitegemee kupokea kitu kutoka
kwao bali katika yote hayo tunafanya kwasababu ndio asili yetu..
nakuhakikishia kwa kufanya hivyo utayafurahia maisha, maana utakuwa huru
bila mizigo ya kubeba watu rohoni mwako. #Badonajifunza
Nina mambo mawiliya kukuambia
1. Wakati mwingine unaweza usijue una uwezo kiasi gani katika hicho unachofanya mpaka umekaa chini na kujifunza kutoka kwa wanaojua/waalimu.. coz unaweza jiona unajua kumbe hujui.. na hiyo ikasababisha ukafanya mambo yasiyokuwa na ubora.
2. Mtu yeyote anaweza kutumiwa na shetani kwa lengo la kukukwaza, kukukasirisha au kukufanya ukose amani ambayo inaweza kukupelekea kujenga chuki/uadui ndani yako ukamkosea Mungu bure, lakini ukiwa mjanja unaweza kutumia hayo makwazo kama moja ya somo la vitendo kukupa uzoefu katika kusamehe.
(Jifunze kujifunza, ufurahie maisha)

