UTARITHISHWA, UTARITHI, UTARITHISHA
Story by; Nemes Mnyanga (Chief)
Nemes akiwa amemshika Gamba
Iliikua alfajiri huku
jua la asubuhi likiwa linachomoza na upepo mzuri ukipuliza miti iliyozunguka
shamba hilo, na sauti za vyura pamoja na ndege wakiipamba kwa sauti zao
maridadi asubuhi ile.
Ndipo mvulana
shupavu na jasiri aliyejengeka vyema mwili kutokana na kazi ngumu ya kukata
magogo ya miti na kuyabeba, Kijana huyo aitwae Nemes Mnyanga alipoonekana akitua
shoka na jembe chini, kisha akatoa fulana kuu kuu aliyokua amevaa akiacha kifua
chake kionekane vyema....
Na hizi shughuli za
kukata mkaa ndizo zilizofanya kijiji chote cha Mandela kimjue na kumpenda kwa ushupavu
wake.
Kama ilivyo siku zote aendazo
kukata magogo, lakini siku hii ilikua tofauti. Wakati anashusha shoka la kwanza
kuelekea kukata mti mkubwa uliokwisha kukauka, akasikia kwa ukaribu takribani
kilomita chache, mwanaume akipiga kelele za kuomba msaada toka shambani, kelele
zilipozidi, akatupa jembe na kuchukua shoka lake kama silaha tayari kuelekea
kelele zinapotokea kukabiliana na hatari anayoweza kukutana nayo.
JE UKO SHAMBANI KIMETOEA NINI?
Akiwa mwenye hamaki na jasho jingi likimtoka japo ilikua ni
alfajiri na kuna ubaridi mkali, lakini kwake ilikua tofauti, alikuwa akipiga
mbio huku mkono wa kulia ameshika shoka lake na mkono wa kushoto anautumia
kuachanisha miti na majani yalisonga njia japo miba ni mingi hakujali,
alichojali ni kumfikia mwanaume huyo ambaye alikuwa akiendelea kupiga mayowe
yenye uchungu mkali na yakiashiria anakata tamaa ya kupata msaada, lakini cha
kushangaza, alipokua anakaribia maeneo ya sauti inapotokea akagundua “My
God! hii si sauti ya GAMBA..!!” Nemes alisikika akishitushwa zaidi na
wasiwasi ukimzidi. Kijana Gamba alikuwa anajishughulisha na kilimo cha mpunga
kwa miaka yote. Ndipo Nemes anavuta pumzi na kuongeza spidi kutokomea katika
shamba la mpunga la kijana Gamba. Hatua chache mbele yake anaona kimbunga
kikubwa kilichokusanya vumbi na majani, kikimuelekea rafiki yake aliyekua chini
akijisogeza kukikimbia kimbunga kile, akionyesha tayari amekwisha ishiwa nguvu
na miguu yake ikiwa na hali ya ganzi,
Wakati Nemes amesimama akitetemeka angali jasho
likimmiminika, akiwa anafikiria atawezaje kumwokoa rafiki yake, tayari kimbunga
kipo karibu nae, hana la kufanya. Alisikika akiita,
Gambaaaaaa….! Nooooo..! Noooo..!
kimbunga kilienda na kumzoa Gamba kikamkusanya na kumtupa
bila huruma katika tope zito pembeni ya shamba lake kasha kikapotea.
Huku Nemes akiwa anakuja mbio akiendelea kuita na machozi na
jasho jingi vikimtoka hakuwa akiamini kinachotokea mbele yake, akitamani
ingekuwa ni ndoto, kwani upendo wake kwa rafiki yake ulikuwa hauna unafki.
Anafika mpaka alipo anguka Gamba na kumuinua upande wa shingo
uku akimuuliza kilichomtokea Gamba,
“Gamba Ga...Gambaaa tafadhali nieleze nini kimetokea…”
lakini Gamba mwenye maumivu makali akihema kwa tabu sana na
akiwa amejawa na udongo mwilini mwake mithili ya mtu aliyefukuliwa chini ya
ardhi alikua awezi kusema zaidi ya kuonyesha jeraha kubwa lililokua likivuja
damu katika mguu wake wa kushoto.
Kutokana na ujasiri wa nemes anafikiri kwa haraka na kumbeba
Gamba tayari kuelekea kijijini,
Nemes anamuinua Gamba anamtia begani bila kusahau shoka lake,
anaanza kukimbia kuelekea kijijini huku rafiki yake akiwa begani akilia kwa
uchungu….,
Jee nini kimemtokea Gamba akiwa shamban na jee itakuaje safari ya nemes
kumrudisha gamba kijijini??
Usikose episode ya pili ya simulizi hii yenye
kusisimua.

Story ni ya ukweli sanaaaa dah
ReplyDeleteDah god stor
ReplyDelete